Michezo
Yanga watangaza kuachana na Juma Kaseja
Klabu ya Yanga imetangaza rasmi kuachana na mlinda mlango wake Juma Kaseja kwa madai kuwa mchezaji huyo hajaonekana klabuni kwa majuma matatu.
Akizungumza mjini Zanzibar leo Mkurugenzi wa Habari wa Yanga, Jerry Muro amesema Kaseja amevunja mkataba kutokana na kutokwenda mazoezini kwa saa 48.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga Jerry Murro akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Unguja