Zlatan na Pogba kuikabili Newcastle
Mshambuliaji wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic na Paul Pogba wanatarajiwa kurejea dimbani siku ya Jumamosi kuikabili Newcastle huko Old Trafford.
Ibrahimovic mwenye umri wa miaka 36 amekuwa nje ya uwanja tangu apate majeraha mwezi Aprili.
Wakati kiungo wa timu hiyo Pogba mwenye umri wa miaka 24 hajacheza mchezo wowote tangu apate majeraha wakati timu yake ilipoikabili klabu ya Basel mwezi Septemba.
Huku mchezaji, Marcos Rojo pia akitarajiwa kuwepo na meneja wa kikosi cha United, Jose Mourinho akisisitiza kuwa wote amewapanga.
Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Sweden, Ibrahimovic huu utakuwa mchezo wake wa 46, huku akiwa amefunga jumla ya mabao 28 ndani ya United msimu uliyopita.
Mourinho amesema Romelu Lukaku atakuwa sambamba na Ibrahimovic hapo kesho.