Burudani
50 Cent aongezewa shavu na Starz, ni baada ya tamthilia ya Power kuwa na mafanikio makubwa
Rapper Curtis “50 Cent” Jackson amesaini mkataba mpya wa miaka miwili na kituo cha runinga cha Starz baada ya tamthilia ya Power anayoitayarisha kupata mafanikio makubwa.
Kupitia mkataba huo, 50 atatengeneza miradi mipya kupitia kampuni yake G Unit Film & Television, Inc. na kuendelea kuwa mtayarishaji mkuu wa tamthilia ya “Power.”
Msimu wa tatu wa Power ulianza kutengenezwa mapema mwezi huu.