Wakishirikiana na kampuni ya kutengeneza vimiminika laini vya CocaCola, MTV Base wataendesha shindano maalumu kwa ajili ya kumpata mtangazaji (VJ) wa televisheni hiyo kwa hapa Tanzania.
Wakishirikiana na kampuni ya kutengeneza vimiminika laini vya CocaCola, MTV Base wataendesha shindano maalumu kwa ajili ya kumpata mtangazaji (VJ) wa televisheni hiyo kwa hapa Tanzania.
Tukio hilo kubwa inasemekana litafanyika kuanzia mwezi Juni mwaka huu kumtafuta mshindi atakayepewa kazi ya kuwa (VJ). Suala la umri ni la kuzingatia kwani wanaotakiwa kushiriki ni wale wenye umri usiozidi 23.
Shughuli hiyo itafanyika katika miji ya Dar es Salaam na Arusha na itarushwa hewani na moja ya vituo vya TV hapa nchini.
Shindano hilo pia litafanyika katika nchi za Afrika Mashariki za Kenya na Uganda kutokana na MTV Base kutaka kupata VJ’s kwenye nchi hizo.