Afande Sele asema amechoka maisha ya ukapera
Baada ya hivi karibuni rapper kutokea Morogoro, Afande Sele kudai kuwa hana mpango wa kufunga ndoa, Jumatano hii ametengua kauli hiyo kwa kudai kuwa amechoka maisha ya ukapera.
Afande Sele akiwa na watoto wake mkubwa anaitwa Tunda na mdogo Sanaa
Rapper huyo ambaye kwa sasa ana jukumu la kuwalewa watoto wake wawili ambao mama yao alishafariki dunia, ameonyesha kuchoshwa na kazi mbalimbali za nyumbani ambazo analazimika kuzifanya.
“Najisikia kuoa tena,” alisema Afande. “Mara chache huamua kula kwenye sufuria kwa sababu naishi mwenyewe hivyo napika mwenyewe, naosha vyombo mwenyewe nk, hivyo kwasababu ya uvivu wangu katika kuosha vyombo wakati flani huamua kula kwenye sufuria ili kuepuka kuchafua vyombo zaid pasi na ulazima,” aliandika kupitia facebook yake.
Hivi karibuni alikaririwa na chombo kimoja cha habari akidai kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kumtafuta mwanamke sahihi ambaye atafanya naye maisha.