Burudani
Baada ya kupotea kwa muda mrefu, msanii wa muziki Craig David arejea kwa kishindo
Kwa watu ambao ni wafuatiliaji wa muziki hususani nyimbo za miaka ya nyuma basi ukitaja jina la Craig David huwezi kuliacha kwenye orodha ya wasanii wa muziki wa R’n’B wakali duniani.
Craig kutoka Uingereza, amerudi kwa kuachia video ya wimbo wake mpya wa MAGIC ambao amemshirikisha Baney Boy.
Kwa mwaka 2018 tayari mkongwe huyo ameachia ngoma mbili mbali na ngoma yake mpya ya Magic, ameachia pia ‘I know You’ na ‘Live in the moment’ .
Craig David alishawahi kutamba miaka ya nyuma na ngoma kama Walking Away, Seven Days na nyingine kali.