Burudani
Baby Madaha akutana na ‘majanga’ bandarini
Baada ya kukamilisha kununua vifaa mbalimbali vya utayarishaji wa filamu kwaajili ya kampuni yake mjini Dubai, Baby Madaha amedai kukutana na changamoto bandarini.
Ameiambia Bongo5 kuwa hali hiyo imesababisha mzigo wake kukaa kwa muda mrefu bandarini hapo.
“Nimekutana na changamoto kubwa sana bandarini,@ amesema. “Kutoa kontena lako mchakato umekuwa mkubwa mpaka umeniharibia ratiba zangu, ni usumbufu tu wa TRA, mara leo wakague kesho utasikia kingine,” amesema Baby Madaha.
“Nashukuru Mungu kuna baadhi ya vitu ambavyo tayari vimeshaingia na natarajia kuanza kazi soon baada ya kukamilisha process zote.”