Michezo
Bado point 3 tu Yanga kutwaa Ubingwa
Mabingwa wa kihistoria Ligi Kuu Tanzania Bara Young Africans Sports Club wamebakiza alama tatu pekee ili kutangaza Ubingwa wa NBC katika msimu huu wa 21/22.
Yanga inaongoza Ligi kwa alama 64 baada ya sare ya leo ya goli 1-1 dhidi ya Biashara United huku mshambuliaji wake Fiston Mayele akifikisha idadi ya mabao 14.