Michezo
BBC kupeleka timu ya watu 272 kuonesha kombe la dunia nchini Brazil
![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2014/04/article-2595844-0B4A782D000005DC-585_634x559.jpg)
Shirika la Utangazaji la Uingereza, BBC litapelekea wafanyakazi 272 kwenye kombe la dunia nchini Brazil katikati ya mwaka huu. Idadi hiyo ni sawa na timu 25 za mpira.
Alan Hansen, Gary Lineker na Alan Shearer watakuwa miongoni mwa timu ya watu 272 ya BBC itakayoenda Brazil
Zaidi ya pauni milioni 12 zitatumika kukava michuano hiyo itakayoanza June 12. Kutakuwepo na timu 12 tofauti za matangazo zitakazoonesha zaidi ya mechi 50 kwenye TV na zaidi ya mechi 60 kwenye redio.
Hata hivyo idadi hiyo ni ya chini ukilinganisha na watu 295 walioenda AfriKA Kusini mwaka 2010.