Burudani
Lupita Nyong’o amshukuru Jay Z kwa kumpa shavu kwenye ‘We Made It’
Ukirushwa na Jay Z kwenye ngoma yake na usishangilie kwa furaha, basi utakuwa na matatizo. Lupita Nyong’o ameamua kutoa neno la shukrani kwa Jay Z na Jay Electronica kupitia Twitter baada ya Hov kumtaja muigizaji huyo wa filamu ya 12 Years A Slave kwenye “We Made It (Freestyle).”
Kwenye ngoma hiyo, Jay Z anasema: “I’m on my Lupita Nyong’o, stuntin’ on stage, after 12 Years A Slave, this Ace of Spades look like an Oscar, Black tux, look like a mobster.”
Kupitia Twitter Lupita ameandika:
Dear Mr. Carter & Mr. Thedford, your shout-out made me screech with glee. Mad BK & NOLA love. #WeMadelt – LN
@S_C_ @JayElectronica
— Lupita Nyong'o (@Lupita_Nyongo) April 2, 2014