Habari
BREAKING: Ndege ya shirika la Ethiopian Airlines yaanguka ikitokea Addis Ababa kwenda Nairobi, watu 157 wahofiwa kufa
Ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia, aina ya Boeing 737 MAX imeanguka leo asubuhi Marchi 10, 2019 ikitokea Addis Ababa, Ethiopia kwenda Nairobi Kenya.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa ndege hiyo ilikuwa na watu 157 na haijulikani imeanguka eneo gani, huku juhudi za kuitafuta zikiendelea mpaka sasa hivi.
Tayari Ofisi ya waziri Mkuu wa Ethiopia, imetuma salamu za rambi rambi kwa familia zilizopoteza ndugu zao kwenye ajali hiyo.