Habari
Bunge lahairishwa rasmi hadi Septemba
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amehairisha vikao vya bunge leo Mjini Dodoma hadi tarehe 5, Septemba saa 3:00 asubuhi ambapo itakuwa siku ya Jumanne.
Waziri Majaliwa ameyazungumza hayo wakati akitoa hoja za Kuhairishwa kwa bunge Mjini humo.
“Naomba kuhairisha Bunge hadi tarehe 5 Steptemba saa 3: 00 asubuhi siku ya Jumanne. Naomba kuwasilisha hoja,” amesema Waziri Mkuu.
Bunge la bajeti lilikuwa takribani kwa miezi mitatu.
Na Emmy Mwaipopo