Rapper Chemical amesema baada ya kusimama mwenyewe sasa ni muda wa kufanya collabo.
Amesema kuwa tayari ameshafanya wimbo na Fid Q na Cliff Mitindo.
Hitmaker huyo wa Sielewi, ameiambia Bongo5 kuwa hakupenda kuanza na kushirikisha wasanii wakubwa kwakuwa alitaka asimame mwenyewe kwanza.
“Mwanzoni nilikuwa naogopa sana kufanya collabo kwasababu watu wengi wangehisi ‘umetolewa na mtu fulani,” amesema.
“Kuna collabo nimefanya na Fid Q, you can’t imagine, Chemical featuring Fid Q. Kuna Cliff Mitindo, kwahiyo ukizisikiliza hizo ladha utajua kabisa itakuwa ni ngoma kali.”