Chris Brown achoka kuandamwa na kesi ya kumpiga Rihanna, adai X ni albam yake ya mwisho
Chris Brown anafikiria kuachana kabisa na muziki siku za usoni na amesema huenda X ikawa albam yake ya mwisho. Breezy ametumia akaunti yake ya Twitter kuelezea kuchoshwa na kuandikwa vibaya kila kukicha kutokana na kosa alilolifanya akiwa na miaka 18 la kumpiga aliyekuwa mpenzi wake Rihanna.
Kupitia Twitter Chris ameandika:
Being famous is amazing when it's for ur music and talent. I'm tired of being famous for a mistake I made when i was 18. I'm cool & over it!
— Chris Brown (@chrisbrown) August 6, 2013
Don't worry mainstream America.After this X album, it'll probably be my last album.
— Chris Brown (@chrisbrown) August 6, 2013
X itakuwa albam ya sita na itatoka mwaka huu akiwa amewashrikisha Kendrick Lamar, Kelly Rowland, Wiz Khalifa, na Rihanna. Hivi karibuni alishoot video ya wimbo wake Love More aliomshirikisha Nicki Minaj.