Burudani
Chris Rock kusherehesha tuzo za Oscar 2016
Mchekeshaji na muigizaji wa Marekani Chris Rock, ametajwa kuwa host wa tuzo za Oscar mwezi February mwakani.
Hiyo itakuwa mara ya pili kusherehesha tuzo hizo za filamu zinazoheshimika kuliko zote duniani.
Tuzo hizo zitatolewa February 28 jijini Los Angeles. Mara ya kwanza Rock alihost tuzo hizo mwaka 2005.