Burudani
Dida kuimba Taarab
Dida pichani, mtangazaji wa redio Times kipindi cha Taarab anatarajiwa kupanda jukwaani kwa mara ya kwanza na kuimba nyimbo moja sambamba na kundi zima la Jahazi Mordern Taarab katika tamasha litakalofanyika Magomeni katika ukumbi wa Traventine Hotel.
Dida hajawahi kuimba taarab hata siku moja, Jumapili ya kesho tarehe 3/10/2010 itakuwa mara ya kwanza kabisa pale Traventine ambapo kundi zima la Jahazi chini ya Mzee Yusuph litakuwa likiendelea kutambulisha album yake ya Valentine na nyimbo zingine mpya kwa wapenzi wake wa Dsm na vitongoji vyake.