Habari
Donald Trump ampa shavu Ben Carson
Rais mteule wa Marekani, Donald Trump ameendelea na kazi ya kuteua viongozi kwenye nyadhifa tofauti tofauti ambao watashirikiana kuiongoza nchi hiyo.
Trump amemteuwa Dkt. Ben Carson ambaye alikuwa mpinzani wake kwenye uchaguzi wa ndani wa chama cha Republican kuwa waziri wa makazi na ustawi wa jamii.
Mpaka sasa Rais huyo ameshafanikiwa kuteuw viongozi kadhaa ambao watashirikiana kwenye safari yake hiyo ya uongozi akiwemo Reince Priebus, Stephen Bannon, Michael Flynn, Jeff Sessions na wengine.
Trump anatarajiwa kuapishwa Ijumaa ya Januari 20, mwakani.