Burudani
Ex wa Ludacris aponda ndoa yake na Eudoxie, asema ni ujanja wa kutaka kumchukua mtoto waliyezaa
Wakati Ludacris na mke wake Eudoxie, raia wa Gabon wanaendelea kufurahia fungate lao, mwanamke aliyezaa na rapper huyo, Tamika Fuller amedai kuwa mzazi mwenzie huyo amefunga ndoa ili kujiwekea mazingira ya kumchukua mtoto wao.
Luda na Tamika wana mtoto wa kike mwenye mwaka mmoja aitwaye, Cai.
Tamika anahofia kuwa nyumba yenye furaha ya Ludacris itampa sifa mahakamani ya kupewa ruhusa ya kukaa na mtoto huyo.
Kwa mujibu wa TMZ, Tamika anaamini kuwa Luda atakuwa na wakati mwepesi wa kuthibitisha kuwa ana mazingira yanayoeleweka na yanamfaa mtoto kuliki yale yenye mama peke yake.
Kwa sasa Ludacris humlipa Tamika $7,000 kila mwezi kama child support.