Mitindo

Face T-Shirt ndiyo habari yao

Ni siku nyingine tunakutana katika habari za mitindo kutoka Bongo5 pekee, kumbuka habari hizi ni kila siku ya Jumapili .

Leo nataka tutazame mtindo unaohusu uvaaji wa T-Shirt, ila hapa ni Face T-Shirt , aina hii ya nguo uvaliwa na jinsia zote na iliwahi kuwepo mika ya zamani kidogo, ila haikuwa imeboreshwa kama ilivyo sasa. Miaka ya zamani zilikuwepo ila zilikuwa hazina rangi za kumvutia mtu.Uzuri wa T-Shirt hizi kwa karne ya sasa inayokwenda na wakati jinsia yoyote anauwezo wa kuvaa.

Jambo la msingi ni kuhakikisha unapata nguo hii iliyo size yako ,uzivae over size kwani sura ya picha ya mtu huyo haitoonekana vizuri, T-Shirt hizi zipo za rangi mbali mbali ila nyeusi na nyupe ndio changuo la watu wengi.

Kumbuka kuvaa T-Shirt hii ni sawa na kuwa shabiki wa picha uliyoivaa hivyo basi ni vizuri kuvaa ya mtu unayempenda. Mafano msanii wa muziki ama muigizaji au nembo ya kitu chochote unachokipenda.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents