Burudani
Flaviana Matata achumbiwa, Russell Simmons ampongeza
Flaviana Matata hayupo tena sokoni. Mwanamitindo huyo wa kimataifa amechumbiwa weekend hii.
Flavy ameshare habari hiyo njema kwenye mtandao wa Instagram kwa kuweka picha inayoonesha kidole chake cha chanda ambacho kimevishwa pete ya uchumba. “I said YES,” aliandika Flavy kwenye picha hiyo.
Mwanzilishi wa label ya Def Jam Records, Russell Simmons aka Uncle Rush ni miongoni mwa watu waliompongeza Flaviana.
“Congratulations to @flavianamatata. Engaged. Pay close attention to the ring fellas u blew it. My Lil daughter supermodel ms Tanzania is off the market lol,” ameandika Russell.