Spika wa Bunge, Tulia Ackson amesema anasubiri uamuzi wa mahakama kuhusu wabunge 19 wa Viti Maalum waliofukuzwa uanachama na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Dk Tulia amesema hayo leo Jumatatu Mei 16, 2022 wakati akitoa maelezo ya wabunge hao ambao walivuliwa uanachama na Chadema.
“Bunge haliwezi kuingilia mchakato huo mpaka Mahakama Kuu itakapotoa uamuzi, ninalazimika kutokutangaza kuwa nafasi za viti maalumu 19 vya Chadema viko wazi mpaka pale mahakama itakapokamilisha kazi yake ya kutoa uamuzi” amesema Dk Tulia