Burudani

GK asema Diva ndiye mpenzi wake bora kuliko wote aliowahi kuwa nao

Rapper wa East Coast Team, King Crazy GK amefunguka na kuweka wazi uhusiano wake wa kimapenzi na mwanadada Diva Loveness Love.

GK1

Akizungumza na kipindi cha Mkasi kupitia EATV Jumatatu (Jan.12), GK alisema Diva ni mpenzi wake bora kuliko wapenzi wake waliopita, huku akidai kuwa mitandao ya kijamii imechangia ku-boost penzi lao.

“inawezekana, kwa sababu ni mwema kwanza halafu na mitandao, unakuta watu wana exchange information, mpenzi wangu wa sasa anazungumziwa sana kwa sababu kuna njia nyingi za kupashana habari” alisema GK.

Baada ya kauli hiyo mwanadada Diva ambae ni mtangazaji wa Ala za Roho ndani ya Clouds Fm, kupitia ukurasa wake wa instagram aliandika: “Aww My baby .. My Gk told ya .. I love him so much .. I love his Charm and his intelligence . best Man On earth.. eeh niambieni kasemaje??”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents