H.Baba adai mke wake amekuwa ‘mrembo’ zaidi baada ya kujifungua mtoto
Msanii wa muziki na filamu nchini H.Baba amesema anawashangaa wale wenye imani kuwa mwanamke akizaa huchoka. Amesema mke wake amekuwa mrembo zaidi baada ya kujifungua miezi mitatu iliyopita kiasi ambacho amejikuta akimtamani zaidi.
Akizungunza na Bongo5 leo H.Baba amesema baada ya kupata mtoto kutoka kwa mke wake, amekuwa mwenye furaha na kumpenda zaidi,.
“Usidanganike wangu,mke wako ukizaa naye unaweza ukahisi kuna kitu kimeongezeka utashangaa unampenda zaidi mimi siamini mwanamke akizaa nachoka.Hivi ninani alisema eti mwanamke akizaa anachoka ni uongo. Mke wangu kazaa amekuwa mzuri zaidi ya zamani, namaanisha namtamani upyaa kama kashushwa leo , na nyumba yetu inaendelea kuwa na amani na upendo daima,” alisema Baba Tanzanite.
Wakati huo H.Baba amesema anatarajia kufanya filamu ya pamoja na mke wake Flora Mvungi pamoja na mtoto wao Tanzanite.
H.baba amesema yeye atacheza kama askari polisi mtenda haki.