Harmonize achafua hali ya hewa mtandaoni, Barnaba na Eugy kutoka Ghana watoa baraka zao (+video)
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Harmonize amekuwa gumzo mitandaoni kwa siku ya leo Tanzania baada ya kutangaza kuwa anaachia ngoma mpya.
Harmonize kupitia ukurasa wake wa Instagram amewaahidi kuwa ataachia video ya wimbo wake mpya endapo atatapata maoni (Comments) zaidi ya 2000.
https://www.instagram.com/p/BmpthRRFyPT/?taken-by=harmonize_tz
Posti hiyo mpaka sasa imeshangaa masaa manne na tayari imefikisha comments 3000+ na views 102,000+ na kinachofuatia sasa ni mashabiki wake kumuandama mitandaoni mkali huyo wa Kwangwaru kuachia kichupa hicho.
Wengine waliotoa neno juu ya ujio wa ngoma hiyo ni mwanamuziki Barnaba na Eugy kutoka nchini Ghana ambao nao wamedai kuwa wimbo huo utakuwa ni moto wa kuotea mbali.
“Aiseee hili chuma, chuma naikumbuka mzee balaa sana ni chuma na nusuu,“ameandika Barnaba huku msanii wa muziki kutoka Ghana, Eugy akiandika “Let’s goooo!!“.
Ngoma hiyo mpya ya Atarudi ni ngoma ya tatu ya Harmonize kufanya kwa mwaka huu baada ya ngoma yake ya DM Chick na Kwangaru aliyomshirikisha Diamond Platnumz kufanya vizuri.
Je, Atarudi huenda ukawa wimbo mkubwa na mkali zaidi ya Kwangwaru na DM Chick?
Good Big
Watasema na comments za insta amenunua
Gud
Bo’s mwengine uyo
Hhhh jamani awa ma brother siamini nguvu wanayo itumia sio ya kawaida mbon wanatish sana
Big support from me broo
Hii ni kiki tuh ya msimu
Ujio wa huyu dogo mi unantia wacwas. C kwa ujio huu
Nakubal
Big support Kondeboy
Yupo good sana