Burudani
Justin Bieber apata ajali ya gari wakati akikwepa camera za mapaparazi
Justin Bieber amepata ajali ya gari jana mchana huko Beverly Hills wakati akiwakwepa mapaparazi waliokuwa wakimfuata.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, msanii huyo alikuwa amekaa kwenye kiti cha abiria kwenye gari aina ya Escalade wakati ajali hiyo inatokea na haraka alihamishiwa kwenye gari nyingine.
Hata hivyo, Hakuna aliyeumia kwenye ajali hiyo.