Habari

Kamanda wa Polisi Arusha apata ajali mbaya ya gari

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo amepata ajali mbaya ya gari katika eneo la Mdori mkoani Manyara baada ya gari alilokuwa akitumia kusafiria kupasuka gurudumu ‘tairi’ ya nyuma na kupoteza muelekeo.

Gari aliyokuwa amepanda Kamanda Charles Mkumbo

Taarifa hizo zilizothibitishwa na mlinzi wa Kamanda Mkumbo kwa njia ya simu ya RPC, amesema Mkumbo amepata ajali hiyo ambapo ndani ya gari aliyokuwa akiitumia walikua watu watatu akiwemo msaidizi wake pamoja na dereva.

ajali.jpg

Kamanda Mkumbo amepelekwa katika hospitali ya Mount Meru mkoani Arusha kwa ajili ya matibabu zaidi huku ikielezwa kuwa ameumia vibaya maeneo ya kichwani.

Chanzo:NIPASHE

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents