Technology

Kampuni ya Google yapigwa faini ya dola bilioni 2.7

Google imepigwa faini ya dola bilioni 2.7 na tume ya ulaya baada ya tume hiyo kudai kuwa kampuni hiyo ilikuwa imekiuka mamlaka yake ya kuweka matangazo yake binafasi kuwa ya kwanza.

Faini hiyo ndiyo kubwa zaidi iliyotolewa na tume ya ulaya hadi leo, kwa kampuni ambayo imelaumiwa kwa kukiuka sheria za biashara.

Amri hiyo pia inataka Google kundoa vizingiti vinavyozuia ushindani ndani ya kipindi cha siku 90 la sivyo ichukuliwe hatua zaidi.

Kampuni hiyo ya Marekani inasema huenda ikakata rufaa.

Tume ya Ulaya ilisema inaiachia Google jukumu la kuamua ni mabadiliko yapi itafanyia mifumo yake ya mauzo.

“Kile ambacho Google imekifanya na haramu chini ya sheria za EU,” alisema Margrethe Vestager, kamishina wa ushindanii wa kibiashara wa tume ya EU.

Tume ya Ulaya imekuwa ikichunguza mifumo ya bioshara ya Google tangu mwaka 2010
Mbunifu wa Android azindua simu mpya

Hata hivyo Microsoft hajatoa tamko lolote kufuatia uamuzi huo baada ya mahasimu hao kufikia makubaliano ya kujaribu kuzuia kesi mahakamani siku za usoni.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents