Bongo Movie
Kanumba Day: Msungu ajitangaza kwamba anadaiwa na Kanumba (Video)
Leo April 7 ni miaka 6 toka afariki staa wa filamu, marehemu Steven Kanumba ambapo ndugu jamaa na marafiki alitembelea katika kaburi la staa huyo na kufanya ibada. Mmoja kati ya wasanii waliotembelea kaburini hapo ni Stanley Msungu ambaye aliwahi kufanya movie 6 na staa huyo ambapo pia alitumia muda huo kwa kutangaza kwamba kuna deni anadaiwa na marehemu na atalilipa siku yoyote.