Habari
Kesi ya mtoto wa Gadafi kusikilizwa Libya
Saif Al islam, ambaye ni mtoto wa marehemu Moammar Gaddafi wa nchini Libya, atasikilizia kesi yake nchini humo.
Haya yamesemwa leo na msemaji kutoka ICC, Luis Moreno Ocampo, ambaye yuko nchini humo akifanya maongezi na wakuu wa nchi hiyo kuhusu kesi hii ya Saif Al islam pamoja na Abdullah Senussi, aliyekua mkwe wa Gaddafi na mkuu wa usalama wa nchi ya Libya. Wawili hao wanatuhuma za mauaji pamoja na kesi za kutozingatia haki za binadamu baada ya maandamano kuanza libya mapema mwaka huu.
ICC imeomba uwepo wao katika kesi hii ili kuhakikisha haki itatendeka.
Msemaji wa serikali ya mpito ya Libya imehakikishia watu wa Libya kwamba Saif na Senussi watasikilizwa kwa kesi ambayo na maamuzi yatakua ni yenye haki.