Habari
Kobe Bryant na mkewe Vanessa waonyesha picha ya kwanza ya mtoto wao wa tatu
Mchezaji wa zamani wa timu ya kikapu ya Lakers ya Marekani, Kobe Bryant na mkewe Vanessa wameonyesha kwa mara ya kwanza picha ya mtoto wa wa tatu.
Mtoto huyo alizaliwa Desemba 5 mwaka huu na kuipa nguvu familia ya Kobe kuwa na watoto watatu wote wa kike.
Picha ya mtoto wa tatu wa Kobe na mkewe Vanessa, Bianka Bella
Mtoto huyo amepewa jina la Bianka Bella Bryant wengine ni Natalia Diamante Bryant, 13, na Gianna Maria-Onore Bryant, 10. Wawili hao waliachana Disemba 2011 lakini waliamua kurudiana tena mwezi Januari 2013.