
Kocha mpya wa Simba mbrazil, Robertinho ameondoka nchini usiku wa kuamkia leo Jumanne kuelekea kwao Brazil.
Kwa mujibu wa Klabu ya Simba, Robertinho amekwenda kwao kwa shughuli binafsi.
“Kocha Mkuu Roberto Oliveira ameondoka usiku huu kwenda nchini kwao Brazil kwa shughuli binafsi za kifamilia na anatarajiwa kurejea nchini mwishoni mwa mwezi huu,”- Simba SC
Tangu Simba kuwa chini ya Robertinho baadhi ya Mashabiki wa timu hiyo wamekuwa hawaridhishwi na namna kikosi chao kinavyocheza licha ya ushindi wanaopata.