Lady Jay Dee

Lady Jaydee atoa siri tano za mafanikio katika jambo ulifanyalo

Mwanadada Judith Wambura aka Lady Jaydee, amefunguka kwa kutoa njia tano zinazoweza kumfanya mtu aweze kufika kwenye mafanikio katika jambo alifanyalo.

404501_10151250606915025_800711642_n

Jaydee amekuwa akiulizwa maswali katika ukurasa wake wa Facebook kuhusiana na njia zinazoweza kumfanya mtu afanikiwe katika shughuli anayoifanya na kwakuwa wengi humwamini yeye kama kioo cha jamii anayeweza kuwa mfano wa kuigwa.

Siri alizozitaja ni pamoja na:

1. Kujiamini Kutoogopa, kuthubutu kufanya kile unachoamini unaweza.
2. Kuipenda kazi unayoifanya hata kama ina kipato kidogo.
3. Kufanya maamuzi sahihi bila kuangalia pembeni.
4. Kuenda kuchukua chako bila kusubiri kuletewa.
5. Kufanya kazi kwa bidii bila kuchoka.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents