Burudani
Lipstick za Rihanna zamalizika saa 3 baada ya kuingia sokoni
Ukiwa na nyota ya kupendwa kama ya Rihanna hakuna biashara utakayofanya isifanikiwe. Lipstick mpya za Rihanna za kampuni ya MAC zimenunuliwa kama njugu na katika muda wa saa 3 tu tangu ziingie sokoni zimeisha.
Juzi muimbaji huyo aliwaambia followers wake wa Twitter kuhusu kuingia sokoni kwa bidhaa hiyo lakini baada ya muda mfupi akawaambia kuwa zimeisha.
‘#SOLDOUT!!!!!!!!!! First shipment sell awf!!! Next shipment isn’t til June!!! Mac girls gone wild!!!… [sic]’ aliandika.
Bei ya lipstick hizo ni kuanzia shilingi 25,000.