Naibu Waziri Ofisi wa Waziri Mkuu, Vijana, Kazi na Ajira, Patrobas Katambi, amesema kwamba zaidi ya bilioni 150 zimekwishatolewa kwa vijana kama mikopo na kusema kama kuna kijana yeyote ambaye hajapata mkopo itakuwa pengine ni Mkenya.
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 18, 2022, bungeni jijini Dodoma, wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalum Sophia Mwakagenda, alilohoji kuhusu vijana kutopata ajira kwa zaidi ya miaka 6 sasa pamoja na kwamba mfumo wa utoaji wa mikopo katika Halmashauri kwa vijana mfumo umewatupa nje.