Habari

Mbivu Mbichi za Sabaya leo

Hukumu ya kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wialaya ya Hai Lengai ole Sabaya na wenzake wawili Silvester Nyegu na Daniel Mbura inatarajiwa kutolewa leo Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Lengai Ole-Sabaya (mwenye suti ya bluu) na washtakiwa wenzake wakiwawamefika mahakamani leo.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Amalia Mushi aliahirisha hukumu hiyo Oktoba Mosi, 2021 baada ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo, kutokamilisha kuandika hukumu hiyo.

Agosti 12 watuhumiwa hao walielezwa kuwa wana kesi ya kujibu baada ya kukamilika ushahidi wa mashahidi 11 wa Jamhuri na vielelezo vinane.

Sabaya alisimamishwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Mei 13, 2021 na Rais Samia Suluhu a ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zilizokuwa zinamkabili.

BY: Fatuma Muna

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents