Burudani

Mikoani walikuwa hawaamini kama sisi ndio tulioimba wimbo ‘Kamatia Chini’- Aika

Msanii wa kundi la Navy Kenzo, Aika, amefunguka na kuzungumzia faida ya tour yao ya ‘Kamatia Chini Tour’ ambayo ilifanyika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.
Navy Kenzo

Akizungumza na Bongo5 Ijumaa hii, Aika amesema tour hiyo iliwasaidia kuwatangaza kwani walikutana na mashabiki wao ambao walikuwa hawaamini kama wao ndio wameimbi wimbo ‘Kamatia Chini’.

“Kuna vitu vingi kama wasanii tumejifunza, next time ili tujirekebishe na kusawazisha makosa yetu na kufanya kitu kikubwa zaidi,” alisema Aika.

“Mapokezi ya ‘Kamatia Chini’ mkoani yalikuwa makubwa sana isitoshe wimbo ulikuwa hata haijafikisha wiki 2, lakini kila mtu alikuwa anaimba, yaani watu walivyosikia wale watu waliyoimba ‘Kamatia Chini’ wamefika, wengine walikuwa wanakataa. Wanasema hawawezi kuwa hawa, lakini sisi tukawaonyesha sisi ni Watanzania na ndiye tuliyoimba ule wimbo,” aliongeza Aika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents