Burudani

Mimi na Diamond tumekutana muda mrefu kabla ya Zari – Huddah Monroe

Mrembo kutokea pande za +254 Nairobi nchini Kenya, Huddah Monroe amesema hakuna chochote kinachoendelea kati yake na Diamond Platnumz.

Mrembo huyo amelazimika kuzungumzia hilo mara baada ya kuonekana kutokuwa karibu zaidi na aliyekuwa mpenzi wa Diamond, Zari The Boss Lady kama hapo awali.

“Lakini yote yanapita , watu wanaongea sana, ooh! Huddah ana kitu na Diamond, kitu ambacho wanadanganya mwisho wa siku. Mimi na Diamond tumekutana muda mrefu kabla ya kukutana na Zari,” Huddah ameiambia Wasafi TV.

Huddah ameendelea kwa kusema kuwa yeye na Zari walikuwa karibu sana na alikuwa akimueleza vitu vingi sana vya vyake na endeapo angetaka kuvieka kwenye mitandao angeweza lakini hawezi kutokana ni rafiki nzuri.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents