Mimi na Tessy hatuzungumzi mambo kuhusu wapenzi wetu – Irene Uwoya
Msanii wa filamu Irene Uwoya amefunguka kuzungumzia ukaribu alionao na aliyekuwa mpenzi wa muimbaji Aslay, Tessy.
Irene Uwoya na mume waka, Dogo Janja
Muigizaji huyo ambaye ni mke halali wa rapa, Dogo Jana amedai yeye akikutana na mama watoto huyo wa Aslay hawazungumzi ishu kuhusu wanaume zao.
Aslay akiwa na aliyekuwa mpenzi wake Tessy.
“Ni mtu ambaye tukikutana tunazungumza mambo ya biashara, lakini ishu zake za mapenzi huwaga sizijui, pia ishu kuhusu mahusiano yake ni privacy, huwa nikikutana naye hatuzungumzi masuala ya mapenzi kwa kwa sababu kila mtu ana wake,” alisema Uwoya.
Aliongeza, “Sijui kwa sasa yupo na nani kwanza hayanihusu kabisa”
Tessy ambaye alibahatika kuzaa mtoto mmoja na Aslay, anadaiwa kutoka kimapenzi na mfanyabishara mkubwa nchini Tanzania aitwae, Sebastian Ndege.
Siyo wapenzi. You are just rapping dogo jinga and nothing else. He is just like your second born. Shame on you
Wanazingua bhana .
Hapa kuna mtu ana achwa
bibi kabisa
Minashangaaga sana iv kweli uyo mshuga mamy anamvuliaga kweli nguo uyo mtoto wajuzi sikama kumtoleya radhi jamni,usani saa mojaa sio dili kabisa.