Tragedy

Mtoto wa miaka miwili amuua mama yake kwa bastola iliyokuwa kwenye pochi

Mwanamke mmoja nchini Marekani ameuawa na mwanae wa kiume mwenye umri wa miaka miwili baada ya mtoto huyo kuishika bastola iliyokuwa kwenye mkoba wake na kujifyatua risasi kwa bahati mbaya.

2456558900000578-2891673-image-a-1_1419985471752

Tukio hilo limemhusisha mwanamke mwenye miaka 29, Veronica J. Rutledge mkazi wa Blackfoot, Idaho nchini Marekani.

245645D500000578-2891673-image-a-10_1419985619565

Kwa mujibu wa polisi, mtoto huyo alikuwa amekaa kwenye toroli la super market ya Walmart na kuingiza mkono kwenye pochi ya mama yake ambapo aliishika bastola iliyolipuka. Mwanamke huyo alikuwa akifanya shopping kwenye supermarket hiyo akiwa na wanae wanne.

Tukio hilo limenaswa kwenye video za ukaguzi kwenye supermarket hiyo na baadhi ya wafanyakazi walilishuhudia. Supermarket hiyo ilifungwa baada ya tukio hilo.

Chanzo: Daily Mail

Related Articles

Leave a Reply

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents