Mwamuzi wa mechi ya Namungo na Yanga afikishwa kwa pilato
Mwamuzi wa kati wa mchezo wa Namungo FC dhidi ya Yanga SC, Abel William kutoka Arusha amepelekwa kwenye Kamati ya Waamuzi ili shauri lake likajadiliwe na kamati hiyo.
Uamuzi huo umekuja baada ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi Kuu kujiridhisha kuwa mchezo husika ulikumbwa na na matukio na maamuzi yalioacha maswali juu ya ya utekelezaji wa sheria 17 za mpira wa miguu.
Kamati imetoa onyo kali kwa wachezaji wa Namungo FC, Jacob Massawe, Lucas Kikoti na Bigirimana Braise ambao kwa nyakati tofauti walionyesha utovu wa nidhamu kwa vitendo na lugha.
Katika hatua nyingine, Kamati imewapongeza wachezaji wa klabu ya Namungo Obrey Chirwa na Abdulmalik Adam Zakaria kwa kuonesha vitendo vya uungwana mchezo ambapo walionekana wakiwazuia wachezaji wenzao wasimzonge na kumtolea lugha chafu mwamuzi.