Burudani
Mwasiti apanga kuachia ngoma ya Hip Hop
Mwasiti amesema Fid Q, Mwana FA pamoja na Godzilla wamemwambia wapo tayari kumwandikia wimbo wa Hip Hop ili na yeye aoneshe uwezo wake katika muziki huo.
Muimbaji huyo alikiambia kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds TV kuwa ana nia ya kubadili muziki wake kidogo ili kupata ladha nyingine.
“Mimi napenda Hip Hop sana, sema sijawahi kujaribu,” alisema.
“Nitajaribu kuachia wimbo kwa sababu nimepata bahati Mwana FA kasema ataniandikia, Fid Q amesema ataniandikia, Nick wa Pili pamoja na Godzilla wapo tayari kuniandikia. Sasa ni mimi tu nikamilishe halafu niseme lini itatoka,” aliongeza Mwasiti.