Burudani
Naj aliwahi kufanya audition ya filamu za Harry Porter na kidogo apate
Naj aliwahi kufanya audition ya filamu za Harry Porter nchini Uingereza.
Muimbaji huyo alikiambia kipindi cha Chill na Sky kuwa alifanikiwa kuingia kwenye mzunguko wa pili.
“Walitangaza kwenye redio kipindi hicho mimi mdogo mama yangu anajua kabisa napenda sana movie. Tulienda pale sasa foleni, walikuwa wanatafuta msichana mmoja sasa wasichana age hiyo hiyo tulienda wengi nakuambia foleni,” alisema.
Anasema pamoja na kuwahi mapema asubuhi alijikuta akifanyiwa audition jioni.
Baada ya siku kibao alipigiwa simu ili kwenda kwenye hatua iliyofuata iliyokuwa na watu wachache zaidi.
“Baada ya hapo ndio hivyo I didn’t get another call back I think uigizaji ni kitu kilichopo zaidi kwenye damu yangu kabla hata ya muziki.”