Burudani
Neema nyingine yamuangukia 2Face Idibia
2Face Idibia asaini dili la tatu kama balozi ndani ya miezi michache.
Hatua hiyo imekuja baada ya wiki iliyopita kupata shahada ya heshima kutoka chuo kikuu cha Igbinedioncha nchini Nigeria na kuwa msanii wa kwanza wa nchi hiyo kupatiwa tuzo ya heshima kama hiyo.
Mwaka 2016 umeonekana kuwa wa neema zaidi kwa hitmaker huyo wa ‘African Queen’ baada ya kusaini mkataba mwingine na kampuni ya simu, Partner Mobile.