Gurumo atoa ushuhuda wa Loliondo
Mwanamuziki mkongwe wa bendi ya msondo ngoma, anayetimiza zaidi ya miaka hamsini kwenye tasnia ya muziki huo wa dansi, ametoa ushuhuda mbele ya Website ya Bongo5 kwamba amepata kikombe cha babu na kimemsaidia.
Mwanamuziki huyo ambaye mnamo mwezi wa nne, aliwahi kulazwa kutokana na ugonjwa wa mapafu kujaa maji, amesema kwamba tangu aliposikia dawa ya babu wa Loliondo akawa anapanga kwenda kupata hicho kikombe kutokana na maradhi yanayomsibu.
Amesema baada ya kupata kikombe hicho maalum kwa babu Mwasapile, hivi sasa afya yake anahisi inaelekea vizuri tofauti na mwanzo kabla ya kwenda.
Hata hivyo mwanamuziki huyo amedai kwamba zaidi ya ugonjwa wa mapafu kujaa maji ambao alilazwa nao katika hospitali ya Muhimbili, muda na wakati kama ule aliolazwa ndugu yetu marehemu Remmy Ongara amesema pia anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo