Burudani

Ninashukuru BASATA wamenielewa na kunisamehe – Shilole

Shilole a.k.a Shishi bybee sasa anaweza kupata usingizi mnono bila mawazo, sababu lile sakata la kusambaa kwa picha zake chafu zilizopigwa wakati akitumbuiza nchini Ubelgiji mwezi uliopita hatimaye limemalizika vizuri.

shishi new-2

Sakata hilo ambalo lilifika hadi bungeni ambapo Naibu Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia alisema serikali ililiagiza Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA kufanya naye mahojiano ili serikali iweze kuchukua hatua.

Muimabji huyo wa ‘Nakomaa na JIji’ ameelezea furaha yake baada ya kusamehewa na BASATA alipoenda kutoa maelezo.

“Leo nimeenda BASATA kwasababu waliniita juzi, kwahiyo nimeenda kusikiliza wito wao, tumeongea nashukuru wamenielewa tumeongea tumeelewana basi hakuna tena ambacho kitu kina tatizo tena hapo kwasababu wale ni wazazi wanatakiwa kumkanya mtu kama mtoto labda” Alisema Shishi bybee

“Tumeelezana pale nini kifanyike nini kisifanyike na kila kitu ambacho kinahusiana na tasnia ya sanaa. Nimewaelezea situation ilivyotokea wamenielewa wameniambia pia niwe mwangalifu katika mavazi, of-course ni kweli kitu kama hicho kinaweza kutokea kwahiyo sisi ni binadamu, nimeshukuru sana kwasababu wameweza kunielewa, basi ni hivyo tu nina furaha kwaajili ya hiyo kitu.” Alimaliza Shilole.

Source: EATV.TV

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents