Habari
NMB YATOA MSAADA WA MADAWATI ZANZIBAR
Benki ya NMB imeendelea kuwa karibu zaidi na jamii inayoizunguka kwa kusaidia kutatua matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii hususani katika sekta ya elimu. Kama ilivyo ada kwa benki ya NMB hutoa sehemu ya faida yake ili kuisaidia jamii. Benki ya NMB imetoa msaada wa madawati yenye thamani ya shilingi milioni 10/- kwa ajili ya shule ya msingi Mangapwani na Bumbwini mjini Zanzibar.