Habari

Okonjo-Iweala aanza kazi rasmi kama Mkuu wa Shirika la Biashara duniani

Mnageria-Mmarekani, Ngozi Okonjo-Iweala, anaanza rasmi kazi kama mkuu mpya wa Shirika la Biahsara Duniani (WTO) Jumatatu ya leo.

Dkt Okonjo -Iwela ambaye ni waziri wa zamani wa fedha na mambo ya nje wa Nigeria, ni mwanamke wa kwanza wa Afrika kuongoza WTO.

Ngozi Okonjo-Iweala amesema kipaumbele chake ni kushughulikia masuala ya afya na athari za kiuchumi zinazotokana na majanga.

Kuna wasiwasi huko Washington na miji mikuu mingine kuhusu sera za biashara za China na jinsi WTO inavyojiandaa kushughulikia masuala hayo.

Dkt Okonjo-Iweala anafahamika kwa kuwa mwana -mageuzi, lakini atakabiliwa na mslahi ya nchi wanachama.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents