Michezo
Picha: Adriano alivyo apewa heshima ya kuwaaga mashabiki wa Inter Milan
Mshambuliaji wa zamani wa Inter Milan, Adriano ambaye alirejea tena San Siro usiku wa December 21 na kupewa heshima ya kuwaaga mashabiki wa klabu hiyo.
Mashabiki ambao walikuwa wamejitokeza kwa wingi wakati Inter Milan ilipokuwa ikicheza na Lazio na kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 na walimshangilia kwa nguvu naye akionekana akiwa na furaha sana.
Adriano ambaye ni raia wa Brazil, kupindi cha nyuma alikuwa ni mchezaji tegemeo wa Inter Milan 2001 hadi 2002 halafu akarejea tena na kuitumikia kuanzia 2004 hadi 2009 alipoondoka na kujiunga Sao Paolo kwa mkopo.