Burudani
Picha: AKA amtumia ex wake DJ Zinhle maua rose 50!
Rapper wa Afrika Kusini, AKA ameonesha kuwa ni mtu mzima baada ya kumtumia ex wake na mama wa mwanae wa kike, maua rose 50.
Pamoja na DJ Zinhle kukanusha kurudiana na AKA, msichana huyo mwenye miaka 32 amedai kuwa wana maelewano mazuri na mzazi mwenzake.
Zinhle alitumia Instagram kuonesha zawadi hiyo kwa kuandika: 50 roses. Thank you @akaworldwide #nowearenotenemies #weareparents #wegrown #familycomesfirst #nowenottogether #chill #BaddestTeam.
Maua aliyopewa Zinhle na AKA
Hiyo imekuja baada ya gazeti la udaku kudai kuwa mastaa hao wamerudiana baada ya AKA kumuacha Bonang Matheba ili kujaribu kusuluhisha tofauti zake na Zinhle.