Habari
Picha: Ibada ya kuaga mwili wa mke wa Waziri Mwakyembe, Bi Linah
Mwili wa aliyekuwa mke wa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe Bi. Linah umefanyiwa ibada ya mwisho katika kanisa la KKT Kunduchi jijini Dar es salaam ikiwa ni maandalizi ya kuusafirisha mwili huo kuelekea mkoani Mbeya kwaajili ya mazishi.
Ndugu jamaa pamoja na viongozi walipata fursa ya kutoa salamu za rambirambi kwa Waziri. Bi Linah alifariki wiki iliyopita baada ya kuugua ugonjwa wa saratani. Angalia picha.
PICHA NA EMMY MWAIPOPO